Watch FIFA World Cup 2026™

LIVE, FREE and EXCLUSIVE

Taarifa ya Habari 1 Agosti 2023

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Waziri Mkuu Anthony Albanese amejibu shtuma za waziri mkuu wa zamani Scott Morrison, kwa kumshtumu kwa kutokuwa na huruma kwa waathiriwa wa mfumo wa Robodebt.


Published

By Gode Migerano

Presented by Gode Migerano

Source: SBS



Share this with family and friends


Waziri Mkuu Anthony Albanese amejibu shtuma za waziri mkuu wa zamani Scott Morrison, kwa kumshtumu kwa kutokuwa na huruma kwa waathiriwa wa mfumo wa Robodebt.


Benki kuu ya Australia ime amua kuto ongeza kiwango cha hela taslim kwa 4.1% kwa mwezi wa pili mfululizo, ikidai kuwa viwango vya juu vya riba vinafanya kazi kupunguza mfumuko wa bei.

Uongozi mpya wa kijeshi nchini Niger Jumatatu umeishutumu Ufaransa kutaka ‘kuingilia kati kijeshi’ ili kumrejesha madarakani Rais aliyeng’atuliwa Mohammed Bazoum, huku mivutano ikiongezeka kati ya Niger na Ufaransa, iliyokuwa mtawala wa kikoloni kwa Niger, na majirani zake.

Rais wa Nigeria Jumatatu alitangaza hatua kadhaa za kukabiliana na kupanda kwa gharama ya maisha, ikiwemo kutoa tani laki mbili za nafaka ya akiba baada ya ghala la chakula kuporwa kaskazini mashariki mwa nchi.

Mirengo ya Kenya Kwanza na Azimio la Umoja inaonekana kuchezeana mchezo wa paka na panya kuhusu mazungumzo ya maridhiano yanayotarajiwa kusuluhisha masuala tata nchini. Hilo ni licha ya Wakenya kuelekeza macho yao yote kwa vinara wa mirengo hiyo miwili Rais William Ruto na Raila Odinga mtawalia—kuhusu juhudi zao kutatua mzozo huo.

Matildas wajinusuru katika kombe la B la kombe la dunia, baada yaku adhibu Canada kwa magoli 4 kwa 0 nakufuzu kama vinara wa kundi hilo mbele ya Nigeria.


Latest podcast episodes

Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Stream now