Watch FIFA World Cup 2026™

LIVE, FREE and EXCLUSIVE

Taarifa ya Habari 1 Mei 2022

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS Swahili

Chama cha Labor kimezindua kampeni yake ya uchaguzi rasmi katika jimbo la Magharibi Australia, ambako kiongozi wa upinzani Anthony Albanese ametoa ahadi kadhaa za uchaguzi mkuu.


Published

By Gode Migerano

Presented by Gode Migerano

Source: SBS



Share this with family and friends


Chama cha Labor kimezindua kampeni yake ya uchaguzi rasmi katika jimbo la Magharibi Australia, ambako kiongozi wa upinzani Anthony Albanese ametoa ahadi kadhaa za uchaguzi mkuu.


Mweka hazina wa taifa Josh Frydenberg amesema kuwachagua wabunge huru, kutaweza sababisha vurugu na matatizo bungeni. Bw Frydenberg ame zindua kampeni yake ya uchaguzi, kwa ajili yakuhifadhi eneo bunge lake la Kooyong jimboni Victoria. Eneo bunge la Kooyong linajumuisha vitongoji vyakifahari kama Kew na Hawthorn, na eneo bunge hilo limekuwa moja ya eneo bunge salama la chama cha Liberal.

Mwili wa aliyekuwa rais wa tatu wa Kenya, Mwai Kibaki, aliyeaga dunia Ijumaa wiki iliyopita, Jumamosi ulizikwa nyumbani kwake katika mji wa Othaya, jimbo la Nyeri, Kaskazini mwa mji mkuu wa Kenya, Nairobi. Marehemu Kibaki alipewa heshima za kijeshi huku akipigiwa mizinga 19, kama njia ya kumuenzi amiri jeshi mkuu wa zamani. Kibaki aliongoza Kenya kati ya mwaka wa 2003 na 2013.

Wachunguzi wa tuhuma za rushwa zinazomkabili Rais wa zamani wa Afrika Kusini Jacob Zuma wamesema kiongozi huyo wa zamani angefanya chochote ambacho familia ya Gupta mzaliwa wa India walitaka afanye kuanzia mwanzoni mwa muhula wake wa kwanza.


Latest podcast episodes

Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Stream now