Watch FIFA World Cup 2026™

LIVE, FREE and EXCLUSIVE

Taarifa ya Habari 11 Juni 2023

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Waziri wa huduma ya wazee Anika Wells amesema kufanya mageuzi katika mfumo wa huduma ya wazee ni binafsi kwake, Bi Wells amesema aliona matatizo tena, alipo fanya ziara ndani ya vifaa vya huduma baada yakuwa waziri wa huduma ya wazee.


Published

By Gode Migerano

Presented by Gode Migerano

Source: SBS



Share this with family and friends


Waziri wa huduma ya wazee Anika Wells amesema kufanya mageuzi katika mfumo wa huduma ya wazee ni binafsi kwake, Bi Wells amesema aliona matatizo tena, alipo fanya ziara ndani ya vifaa vya huduma baada yakuwa waziri wa huduma ya wazee.


Chama cha The Greens kime sema serikali ya Albanese "inakataa kutingika" katika mashauriano kuhusu mfuko wao wa Housing Australia Future Fund. Mjadala kati ya vyama hivyo viwili uta anza tena wiki ijayo ndani ya seneti, ambako chama cha Greens kinatumai kupata makubaliano kwa kusitishwa kwa muda kwa ongezeko ya kodi za nyumba pamoja na uwekezaji wa ziada kwa nyumba za bei nafuu.

Wakazi wameripoti hali ya utulivu katika mji mkuu wa Sudan Khartoum Jumamosi tangu kuanza kutekelezwa makubaliano ya kusitisha mapigano kwa saa 24 kati majenerali wawili wanaopigana, lakini watu wachache wanaamini kuwa sitisho la mapigano litadumu.

Watu wanaoshukiwa kuwa wanamgambo wa Kiislamu waliwaua watu 12 kuho mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Alhamisi jioni, kulingana na maafisa wa wilaya ya Beni katika jimbo la kivu Kaskazini.

Hatimae Pep Guardiola, iongoza Manchester City kupata ubingwa wa klabu bingwa barani Ulaya.


Latest podcast episodes

Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Stream now