Taarifa ya Habari 11 Juni 2023

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Waziri wa huduma ya wazee Anika Wells amesema kufanya mageuzi katika mfumo wa huduma ya wazee ni binafsi kwake, Bi Wells amesema aliona matatizo tena, alipo fanya ziara ndani ya vifaa vya huduma baada yakuwa waziri wa huduma ya wazee.


Chama cha The Greens kime sema serikali ya Albanese "inakataa kutingika" katika mashauriano kuhusu mfuko wao wa Housing Australia Future Fund. Mjadala kati ya vyama hivyo viwili uta anza tena wiki ijayo ndani ya seneti, ambako chama cha Greens kinatumai kupata makubaliano kwa kusitishwa kwa muda kwa ongezeko ya kodi za nyumba pamoja na uwekezaji wa ziada kwa nyumba za bei nafuu.

Wakazi wameripoti hali ya utulivu katika mji mkuu wa Sudan Khartoum Jumamosi tangu kuanza kutekelezwa makubaliano ya kusitisha mapigano kwa saa 24 kati majenerali wawili wanaopigana, lakini watu wachache wanaamini kuwa sitisho la mapigano litadumu.

Watu wanaoshukiwa kuwa wanamgambo wa Kiislamu waliwaua watu 12 kuho mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Alhamisi jioni, kulingana na maafisa wa wilaya ya Beni katika jimbo la kivu Kaskazini.

Hatimae Pep Guardiola, iongoza Manchester City kupata ubingwa wa klabu bingwa barani Ulaya.

Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service
Taarifa ya Habari 11 Juni 2023 | SBS Swahili