Watch FIFA World Cup 2026™

LIVE, FREE and EXCLUSIVE

Taarifa ya Habari 13 Machi 2022

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS Swahili

Kiongozi wa New South Wales Dominic Perrottet, amesema kutakuwa tathmini kuhusu majibu kwa mafuriko katika maeneo ya kaskazini mashariki ya jimbo hilo.


Published

By Gode Migerano

Presented by Gode Migerano

Source: SBS



Share this with family and friends


Kiongozi wa New South Wales Dominic Perrottet, amesema kutakuwa tathmini kuhusu majibu kwa mafuriko katika maeneo ya kaskazini mashariki ya jimbo hilo.


Takriban tani 1,100 ya taka ime ondolewa kutoka mto Brisbane, wiki mbili baada ya mji huo kufurika. Mweka hazina wa Queensland, Cameron Dick amesema mamlaka wanarejesha bandari ya Brisbani, taratibu katika hali yake yakawaida ya kazi.

Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta Jumamosi alimuidhinisha rasmi mpinzani wake wa zamani wa kisiasa kushika wadhifa wa juu zaidi wa nchi hiyo, Raila Odinga, wiki kadhaa baada ya vyama vyao kuungana pamoja kabla ya uchaguzi wa rais na bunge wa mwezi Agosti mwaka huu. Tangazo hilo lilijiri baada ya naibu wa Rais wa nchi hiyo William Ruto, ambaye pia ana nia ya kugombea kiti cha urais, kutimuliwa kutoka kwa chama cha Jubilee. Ruto, aliyehamia chama cah United Democratic Alliance, UDA, anatajwa na wachambuzi kama mpinzani mkuu wa Odinga, kwelekea kwa uchaguzi wa mwezi Agosti.

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi (UNHCR) linaripoti ukame nchini Somalia unasababisha mzozo wa kibinadamu na ukosefu wa makazi. UNHCR inasema maelfu ya watu wanakimbia maeneo yenye ukame wakitafuta ardhi yenye rutuba na misaada ya kibinadamu ili kuweza kujinusuru kimaisha.


Latest podcast episodes

Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Stream now