Taarifa ya habari 13 Septemba 2020

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS Swahili

Waziri wa afya wa taifa Greg Hunt amesema anaendelea kuwa na imani kuwa, chanjo ya coronavirus itatolewa kwa wa Australia katika nusu ya kwanza ya mwaka ujao.


Jeshi la mapinduzi nchini Mali limeapa kuunda serikali ya mpito ya muda wa miezi 18 ili kuirejesha nchi hiyo katika utawala wa kiraia baada ya mapinduzi ya mwezi uliopita dhidi ya serikali ya rais Ibrahim Boubacar Keita lakini viongozi maarufu wamekataa kuendelea kwa ushawishi wa kijeshi nchini humo.

Waokoaji wanachimba vifusi kufuatia kuporomoka kwa mgodi wa dhahabu nchini DR Congo na kuwawacha watu takriban 50 wakiwa wamefariki. Mgodi huo uliopo karibu na mji wa Kamituga , mashariki mwa taifa hilo uliporomoka siku ya ijumaa kufuatia mvua kubwa.

Viongozi wa Tanzania na Uganda hatimaye wamekubaliana kuhusu ujenzi wa bomba la mafuta linalotarajiwa kujengwa kutoka mji wa Hoima nchini Uganda hadi changalieni mjini Tanga Tanzania.


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service
Taarifa ya habari 13 Septemba 2020 | SBS Swahili