Watch FIFA World Cup 2026™

LIVE, FREE and EXCLUSIVE

Taarifa ya Habari 14 Agosti 2022

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Kaimu waziri mkuu Richard Marles amesisitiza kuwa bado kuna uwezekano wakuboresha mahusiano na China, licha ya ongezeko ya mivutano katika kanda hilo kwa sababu ya Taiwan.


Published

By Gode Migerano

Presented by Gode Migerano

Source: SBS


Share this with family and friends


Kaimu waziri mkuu Richard Marles amesisitiza kuwa bado kuna uwezekano wakuboresha mahusiano na China, licha ya ongezeko ya mivutano katika kanda hilo kwa sababu ya Taiwan.


Mamepa hii leo watu waliondolewa katika uwanja wa ndege wa Canberra, baada ya ripoti za milio ya risasi kusikika katika sehemu ambako abiria hupumzika wakisubiri kuabiri ndege. ACT Police imesema mwanaume mmoja alikamatwa katika sehemu la tukio na bunduki kuchukuliwa, na mtu ambaye amekamatwa ina aminiwa kuwa ndiye mtu pekee anaye wajibika kwa tukio hilo.

Meli ya kwanza ya nafaka inayoelekea barani Afrika kutoka nchini Ukraine tangu uvamizi wa Russia mwezi Februari mwaka huu ilitia nanga katika bandari ya Pivdennyi, jana Ijumaa, waziri wa miundombinu wa Ukraine alisema.

Wakenya wanaendelea kusubiri matokeo rasmi ya uchaguzi wa rais kutoka kwa tume ya uchaguzi na mipaka ya nchi hiyo, IEBC, siku tano baada ya kushiriki zoezi la kumchagua rais, magavana, wabunge na wawakilishi wengine. Hii ni kufuatia uchaguzi uliofanyika Jumanne wiki hii katika taifa hilo la Afrika Mashariki.Hii ni kufuatia uchaguzi uliofanyika Jumanne wiki hii katika taifa hilo la Afrika Mashariki.


Latest podcast episodes

Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Stream now