Taarifa ya habari 14 Machi 2021

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS Swahili

Chama cha Labor cha Magharibi Australia, kimeshinda kwa urahisi muhula mwingine kusalia serikalini, naku ondoa sehemu kubwa ya upinzani wa chama cha Liberal ndani ya bunge la jimbo hilo.


Kaimu kiongozi wa jimbo la Victoria, amesema ni vizuri kuona kiongozi wa jimbo hilo Daniel Andrews akihamishwa kutoka kitengo cha wagonjwa mahtuti nakupelekwa katika chumba kingine cha wagonjwa hospitalini. Bw Andrews alitereza kwenye ngazi zilizo kuwa na mji mapema mwezi huu, nakunja mbavu kadhaa pamoja nakupata jeraha katikati ya uti wa mgongo wake.

Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa amekanusha habari zilizoenea kwa karibu wiki nzima sasa kwamba Rais John Magufuli ni mgonjwa, akisema kuwa rais “ni mzima na anaendelea na kazi zake kama kawaida”. Majaliwa ambaye alikuwa akizungumza wakati wa sala ya Ijumaa mjini Njombe, kusini mwa Tanzania aliwataka Watanzania kupuuza ripoti zinazosambaa ambazo zinaeleza kuwa kiongozi wao ni mgonjwa.

Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imeahirisha kampeni ya chanjo ya AstraZeneca dhidi ya Covid-19, ikifuata mfano wa nchi nyingine kadhaa zilizochukua kama hiyo. Hayo ni kwa mujibu wa taarifa ya serikali ya nchi hiyo. Serikali ya nchi hiyo ilipokea dozi milioni 1.7 ya chanjo hiyo inayotengenezwa na kampuni ya AstraZeneca ya Uingereza na Sweden, na ilitarajiwa kuanza zoezi la kuwachanja watu Jumatatu ya tarehe 15 Machi.

 


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service