Taarifa ya Habari 14 Mei 2023

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Pendekezo la upinzani wa shirikisho kuruhusu wanao pokea malipo ya ustawi kufanya kazi kwa muda mrefu zaidi, kabla wapoteze malipo yao limekosolewa kama wazo lisilo na mashiko.


Meya wa mji wa Brisbane ame ahidi kuwekeza $1 milioni, kusaidia kugeuza kifaa cha karantini kuwa makaazi ya dharura ya wasio na mwakaazi. Meya Adrian Schrinner amesema uwekezaji huo kutoka bajeti ya halmashauri ya jiji, utaelekezwa kwa vifaa vya kufulia katika eneo la Pinkenba lenye vitanda 500, pamoja na usafiri na huduma za maktaba.

Kifaa cha kupandikiza mioyo ya watoto, kime anzishwa jimboni New South Wales. Kiongozi wa NSW Chris Minns ametoa tangazo hilo nje ya hospitali ya watoto ya Westmead, ambako mradi huo uta simamiwa.

Jeshi la Sudan linalopigana na kikosi cha RSF watarejea kwenye meza ya mazungumzo siku ya Jumapili, mwanadiplomasia mwandamizi wa Saudia Arabia alisema hayo huku mashambulizi ya anga na mapigano makali yakiendelea usiku kucha kuzunguka Khartoum licha ya makubaliano ya kuwalinda raia.

Wachunguzi nchini Kenya wamefukua miili mingine 29 siku ya Ijumaa na kufanya idadi ya waathirika wanaohusishwa na ibada ya kutokula wakiamini siku ya kiama imekaribia kufikia 179, ambapo wengi wao ni watoto.

Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service