Taarifa ya Habari 14 Novemba 2023

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Serikali ya shirikisho imesema inapanga kufanya mfumo wa ustawi wa Australia kuwa waki "utu" zaidi, baada ya ripoti mhimu ya tume yakifalme kwa mfumo wa Robodebt kutolewa.


Takwimu mpya zamakaazi zina onesha soko la nyumba zakupanga nchini Australia lina endelea kuwa baya, wakati uhaba wa nyumba zaku panga unasambaa hata katika sehemu za kandani na bei za nyumba zakupanga zikiendelea kuongezeka kuliko ukuaji wa mshahara.

Utafiti mpya umepata kuwa vijana chini Australia, wanataka haki yakuwa katika mazingira ya afya nzuri iwekwe ndani ya sheria, kuambatana na viwango vilivyo wekwa ng'ambo. Utafiti huo kutoka shirika la Australian Conservation Foundation, ume pata kuwa watu 9 kati ya 10 wenye miaka kati ya 13 hadi 24 nchini Australia, wanata Australia ifuate mfano wa zaidi ya nchi 160 duniani ambazo zime fanya geuzi hilo katika sheria zao.

Somalia imesema Jumapili kwamba mafuriko kutokana na mvua kubwa zinazonyesha yameua takriban watu 31 kwenye maeneo tofauti ya nchi. Karibu watu nusu milioni wamelazimika kuhama makwao kutokana na mafuriko nchini humo, huku maisha ya wengine milioni 1.2 yakiathiriwa, waziri wa Habari Daud Aweis amesema wakati akizungumza na wanahabari mjini Mogadishu.

Rais wa Kenya William Ruto Jumatatu wakati wa ufunguzi wa kikao kinachofanyika mjini Nairobi amesema kwamba wadau wa mkataba wa kwanza wa kimataifa wa kuzuia uchafuzi wa plastiki, wanahitaji kuharakisha mchakato huo.

Uganda inalilaumu kundi la ADF ambalo lina uhusiano na kundi la Islamic State kwa mauaji ya watalii waliokuwa kwenye fungate, wakiwa na muongozaji wao katika eneo pamoja na shambulio la shule lililosababisha vifo vya watu 42, wengi wao wakiwa wanafunzi. Waendesha mashtaka nchini Uganda wamemfungulia mashtaka kamanda wa kundi la wanamgambo wanaohofiwa kwa ugaidi na mauaji ya watalii wawili wa kigeni pamoja na dereva wao mwezi uliopita.

Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service