Taarifa ya Habari 15 Februari 2022

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS Swahili

Kiongozi wa jimbo la New South Wales Dominic Perrottet, amesema anatumai kufukia makubaliano na wafanyakazi wa mstari wa mbele wanao andamana.


Maafisa wa afya wa Queensland wamesema shinikizo dhidi ya mfumo wa hospitali za jimbo hilo, inaanza kupungua. Jimbo hilo limepata sehemu ya mwisho ambako ujenzi wa hospitali saba, utafanywa kuanzia baadae mwaka huu. Hali hiyo imejiri wakati jimbo la Queensland, limerekodi kifo cha sita cha UVIKO-19 pamoja na kesi mpya 3,750 za maambukizi.

Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Johnson amemhimiza Rais wa Urusi Vladimir Putin kurudi nyuma kutoka eneo hatari la kukaribia kutumbukia vitani, huku akitahadharisha kwamba uvamizi wa Ukraine unaweza kufanyika katika kipindi cha saa 48 zijazo. Johnson ameieleza hali katika mpaka wa Ukraine kuwa ngumu na ya hatari kubwa huku akiwataka washirika wa Magharibi kusimama pamoja kuonesha mshikamano na nchi hiyo.

Mkuu wa Baraza la Utawala la Sudan Jenerali Abdel Fattah Burhan amekutana na Mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika Moussa Faki Mahamat mjini Khartoum Jumapili kujadili masuala ya kisiasa nchini Sudan. Mtaalamu wa masuala ya uhusiano wa kimataifa wa Sudan, Dr al-Rasheed Ibrahim amesema makubaliano yoyote au juhudi zitasaidia mkakati wa uthabiti wa Afrika. Faki pia atakutana na vyama vya upinzani kusikiliza na kujadiliana nao kuhusu mtazamo wao katika ziara yake ya siku mbili nchini humo.


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service
Taarifa ya Habari 15 Februari 2022 | SBS Swahili