Watch FIFA World Cup 2026™

LIVE, FREE and EXCLUSIVE

Taarifa ya Habari 15 Machi 2022

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS Swahili

Australia na Uholanzi zime zindua hatua zakisheria dhidi ya Urusi kwa kuangusha ndege ya M-H-17 ya Malaysia katika mwaka wa 2014.


Published

By Gode Migerano

Presented by Gode Migerano

Source: SBS



Share this with family and friends


Australia na Uholanzi zime zindua hatua zakisheria dhidi ya Urusi kwa kuangusha ndege ya M-H-17 ya Malaysia katika mwaka wa 2014.


Upinzani wa shirikisho umesema serikali haifanyi vyakutosha kupunguza gharama ya shinikizo ya maisha, wakati uvumi unaendelea kama serikali ita kata kodi ya mafuta. Hata hivyo Waziri Mkuu Scott Morrison amesema uamuzi wa serikali ya shirikisho kwa kodi ya mafuta, hauta tangazwa hadi bajeti ya taifa itakapo tangazwa 29 Machi 2022.

Ujumbe wa Ukraine na Russia umeanza tena mazungumzo ya amani Jumatatu, siku moja baada ya Rashia kufanya shambulio baya la kombora kwenye kambi ya kijeshi magharibi mwa Ukraine, kilomita 25 tu kutoka Poland, mwanachama wa NATO. Watu 35 waliuawa na wengine 134 kujeruhiwa katika shambulio hilo kwenye kituo cha kimataifa kwa ajili ya kulinda amani na usalama.

Kiongozi wa eneo lenye mamlaka ya kiasi, Somaliland, Muse Bihi Abdi ameitaka jumuiya ya kimataifa kulitambua eneo lake kama taifa huru, akisema mazungumzo na Somalia yameshindwa kuzaa matunda. Kiongozi huyo amesema katika mazungumzo yaliodumu kwa muongo mmoja, Somalia imeonesha hali ya kutokuwa na hamasa ya majadiliano yenye tija, na hivyo kuilazmisha Somaliland kuoimba utambuzi wa kimataifa wa kuwa taifa huru.


Latest podcast episodes

Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Stream now