Taarifa ya Habari 15 Mei 2022

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS Swahili

Waziri Mkuu Scott Morrison ame ahidi sera mpya ya makaazi, katika kampeni ya uzinduzi ya chama cha Liberal mjini Brisbane.


Wakati huo huo upinzani wa shirikisho umesema sera ya serikali ya Morrison kwa nyumba, utafanya nyumba ziwe ghali zaidi. Msemaji wa chama cha Labor kwa maswala ya makaazi na ukosefu wamakaazi Jason Clare, amesema mengi yanastahili fanywa kushughulikia swala la makaazi yakijamii na makazi ya gharama nafuu.

Mgombea wa urais katika uchaguzi mkuu wa Kenya, Dkt William Samoei Ruto, amemtangaza mgombea wake mwenza kuwa ni Rigathi Gachagua. Bw Gachagua alikuwa anawania wadhifa huo dhidi ya Profesa Kithure Kindiki, wawili hao wataongoza mrengo wa Kenya Kwanza katika uchaguzi mkuu dhidi ya mrengo wa Azimio One Kenya unao ongozwa na Raila Odinga anaye tarajiwa kumtangaza mgombea mwenza Jumatatu 16 Mei 2022.

Serikali ya Tanzania imetangaza kupandisha kima cha chini cha mshahara wa wafanyakazi wa umma nchini humo kwa 23.3%. Rais wa taifa hilo la Afrika Mashariki, Samia Suluhu Hassan amesema ameridhia mapendekezo ya nyongeza ya mshahara yaliyo wasilishwa Ikulu, ikiwa ni muendelezo wa kikao cha Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ambaye alipokea taarifa ya watalaamu mjini Dodoma kuhusu suala la nyongeza ya mshahara.


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service
Taarifa ya Habari 15 Mei 2022 | SBS Swahili