Taarifa ya habari 17 Novemba 2020

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS Swahili

Chama cha upinzani cha elezea wasi wasi, kuhusu serikali kujaribu kukwepa kuwajibika kwa mfumo tata wakudai madeni.


Joe Biden ametoa angalizo kuwa "watu wanaweza kufa" kama rais aliye madarakani ataendelea kuwa kuzuizi. Akizungumza mjini Delaware, rais mteule alisema ushirikiano aliokuwa anauhitaji ni kukabiliana na mlipuko wa janga la corona.

Viongozi wa nchi za Afrika wameanza Jumatatu juhudi za kutafuta suluhisho kwa mzozo unaozidi kuongezeka nchini Ethiopia, siku mbili baada ya roketi kushambulia mji mkuu wa Eritrea na kuzusha hofu kwamba ugomvi huwenda ukaenea. Rais Yoweri Museveni wa Uganda amekutana na naibu waziri mkuu, ambae pia ni waziri wa mambo ya nje wa Ethopia, Demeke Mekonnen hii leo mjini Gulu, Kaskazini mwa Uganda, kuzungumzia hali ya huko Tigray.

Shirika la kutete haki za kibinadamu nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo ACAJ, linataka maafisa wa usalama nchini humo kumwachilia huru mwanamziki maarufu Tshala Muana ambaye alikamatwa jumatatu mjini Kinshasa. Polisi wamemkamata mwanamziku huyo mweye umri wa miaka 62 baada ya kutoa wimbo ambao wachambuzi nchini humo wanasema kwamba tafsiri yake inamdalilisha rais wa sasa Felix Tshisekedi, japo wimbo huo hautaji mtu yeyote.

 


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service