Watch FIFA World Cup 2026™

LIVE, FREE and EXCLUSIVE

Taarifa ya Habari 17 Novemba 2023

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Waziri Mkuu Athony Albanese ashiriki katika mkutano wa APEC ambako mabadiliko ya hali ya hewa na nishati mbadala ni miongoni mwa mada za majadiliano.


Published

By Gode Migerano

Presented by Gode Migerano

Source: SBS



Share this with family and friends


Waziri Mkuu Athony Albanese ashiriki katika mkutano wa APEC ambako mabadiliko ya hali ya hewa na nishati mbadala ni miongoni mwa mada za majadiliano.


Upinzani wa shirikisho waendelea kuikosoa serikali ya Labor, kwa kutochukua hatua thabiti zaku linda umma na waathiriwa wa wahalifu wanao achiwa huru baada ya hukumu ya mahakama ya upeo.

Waziri wa Afya atangaza uwekezaji mpya zaidi ya milioni mia moja zitakazo tumiwa kuwaajiri zaidi ya wauguzi 100 watakao wahudumia wagonjwa wenye saratani kote nchini.

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa Jumatano lilitoa wito wa “kuongezwa muda wa kusitisha mapigano kwa ajili ya kibindamu” huko Ukanda wa Gaza. Baraza hilo likiachana na majuma kadhaa ya kutochukua hatua na mabishano, hasusani kwa ajili ya ulinzi wa watoto, lakini Israel haraka imekataa hatua hiyo.

Wabunge nchini Kenya Alhamisi wameidhinisha hatua ya kupeleka maafisa polisi 1000 nchini Haiti. Operesheni iliyoidhinishwa na Umoja wa Mataifa, kwa lengo la kulisaidia taifa hilo la Caribbean, kukabiliana na tatizo la ghasia za magenge. Mwezi Julai Kenya iliahidi kupeleka maafisa 1,000 wa polisi nchini humo, baada ya ombi la kimataifa la Haiti la maafisa wa usalama, ili kusaidia katika kukabiliana na magenge yanayolaumiwa kueneza uhalifu.


Latest podcast episodes

Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Stream now