Waziri wa waAustralia wa kwanza Linda Burney amesema, the Voice to Parliament ni suluhu ya vitendo kwa maswala yanayo waathiri zaidi wa Australia wa kwanza, kauli hiyo imejiri baada ya kuungwa mkono kwa kura ya maoni ya Voice ilishuka hadi chini ya 50% kwa mara ya kwanza wiki iliyopita.
Mkurugenzi mtendaji wa sekta ya nyumba za jamii, amesema ni mhimu kufanya kazi na huduma za misaada, kuhakikisha watu wenye mahitaji ya ziada wanapewa msaada katika nyumba za jamii.
Viongozi kutoka nchi saba za Afrika walimuambia Putin kwamba, vita vinadhuru dunia nzima. Ujumbe huo ulikutana na Putin siku moja baada ya kukutana na rais wa Ukraine, Volodymyr Zelensky mjini Kyiv.
Wanamgambo wa kundi la ADF wenye uhusiano na kundi la Islamic State waliua wanafunzi 41 na kuteka nyara wengine sita katika shambulio kwenye shule kaskazini mwa Uganda karibu na mpaka na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, jeshi lilisema Jumamosi.