Taarifa ya habari 18 Oktoba 2020

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS Swahili

Wakazi wa jimbo la Victoria waregezewa vizuizi kwa jiji la Melbourne na maeneo yakanda.


Kiongozi wa chama cha upinzani cha shirikisho anaihamasisha serikali itoe pendekezo la muswada kwa tume ya uadilifu yakitaifa. Mwanasheria mkuu Christian Porter amesema pendekezo hilo la muswada, kwa tume hiyo litatolewa hivi karibuni.

Waziri Mkuu wa New Zealand Jacinda Ardern Jumamosi ameshinda uchaguzi mkuu kwa kishindo, kwa kupata ushindi wa waliowengi.

Maandamano yanatarajiwa kufanyika katika miji kadhaa nchini Ufaransa leo, kuonyesha mshikamano dhidi ya kisa cha kuchinjwa kwa mwalimu aliyewaonyesha wanafunzi vibonzo vya Mtume Mohammed. Kisa cha mwalimu huyo wa historia Samuel Paty kukatwa kichwa nje ya shule viungani mwa mji wa Paris Ijumaa iliyopita, kimeibua ghadhabu nchini Ufaransa na kukumbusha wimbi la machafuko ya Waislamu wenye itikadi kali ya mwaka 2015, ambayo pia yalichochewa na kuchapishwa kwa vibonzo vya Mtume Mohammed kwenye jarida la Charlie Hebdo.


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service
Taarifa ya habari 18 Oktoba 2020 | SBS Swahili