Taarifa ya Habari 18 Oktoba 2022

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Waziri wa Afya Mark Butler, ame ahidi kuwa madai ya ulaghai yaliyo enea kuhusu mfumo wa medicare yanachukuliwa hatua ipaswayo.


Serikali ya Victorian inatoa msaada kwa shule zote shule za chekechea zikijumuishwa katika maeneo ambayo yame athiriwa na mafuriko. Familia zitaweza watuma watoto wao wenye kati ya miaka 3 hadi 4 kupokea huduma yamalezi ya watoto bure katika mhula wa tatu. Wanafunzi wanao jiandaa kufanya mitihani ya V-C-E, wataweza tumia matokeo ya mtihani maalum katika mitihani yao.

Vyombo vya habari vya Uganda pamoja na wanaharakati wa kutetea haki za binadamu Jumatatu wamewasilisha shauri mahakamani kupinga sheria mpya yenye utata kuhusu matumizi ya intaneti, ambayo wanasema inalenga kuzuia uhuru wa kujieleza na kuwanyamanzisha wapinzani. Kulingana na ombi hilo, serikali imepewa siku saba kuwasilisha utetezi wake lakini haijulikani lini kesi hiyo itaanza kusikilizwa.

Rais wa Kenya Dr Ruto, amevunja kikosi cha 'polisi wauaji'. Hatua hiyo inajiri baada ya kiongozi huyo kupokea ripoti ya uchunguzi kuhusu kutoweka kwa raia wawili wa India na mwenyeji wao aliyekuwa dereva wa gari walimokuwa. Ripoti hiyo ilipendekeza kuvunjiliwa mbali kwa kitengo hicho ili kuruhusu uchunguzi kukamilika kabla ya faili hiyo kuwasilishwa kwa mkurugenzi mkuu wa mashtaka nchini kenya.



Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service
Taarifa ya Habari 18 Oktoba 2022 | SBS Swahili