Taarifa ya Habari 1Juni 2021

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS Swahili

Mamlaka ya Afya jimboni Victoria, waongeza kasi kutambua walio jumuika na watu wenye virusi vya COVID-19, baada ya vipimo kufichua ongezeko ya visa vipya jimboni humo.


Mfanyakazi katika meli iliyo tia nanga kusini mwa Perth, amepatwa na COVID-19. Mwanaume huyo mwenye umri wa miaka 20, ina aminiwa ni mpishi katika meli hiyo na, alisafirishwa katika karantini ya hoteli kwa gari la dharura jana usiku kutoka kituo cha Kwinana Bulk Terminal. Kiongozi wa jimbo hilo Mark McGowan amesema zaidi ya idadi ya wafanyakazi 20 ndani ya meli hiyo, kwa jina la Allegra, hawaja onesha dalili zozote za virusi hivyo.

Watu angalau 55 waliuawa katika mashambulizi mawili ya usiku kucha kwenye vijiji huko mashariki mwa Congo, Umoja wa Mataifa ulisema Jumatatu katika usiku ambao ulikuwa mbaya sana kwenye eneo ambalo limeshuhudia ghasia katika kipindi cha takriban miaka minne.

Rais wa Burundi Evariste Ndayishimiye amesema nchi yake iko tayari kuimarisha ushirikiano wake na Kenya pamoja na jamii ya kimataifa. Na Tanzania na Kenya zimetia saini makubaliano ya kuondoa vikwazo vya kibiashara ambavyo vilikuwa vikizuia ushirikiano mzuri wa kufanya biashara.


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service
Taarifa ya Habari 1Juni 2021 | SBS Swahili