Watch FIFA World Cup 2026™

LIVE, FREE and EXCLUSIVE

Taarifa ya Habari 2 Aprili 2023

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Kiongozi wa Victoria amesema kushindwa kwa chama cha Liberal katika chaguzi dogo la Aston, kume onesha wapiga kura wanaendelea kutupilia mbali aina chafu ya siasa.


Published

Presented by Gode Migerano

Source: SBS



Share this with family and friends


Kiongozi wa Victoria amesema kushindwa kwa chama cha Liberal katika chaguzi dogo la Aston, kume onesha wapiga kura wanaendelea kutupilia mbali aina chafu ya siasa.


Kiongozi mpya wa New South Wales Chris Minns amesema haamini hali ya serikali ya wachache ya chama cha Labor itakuwa kizuizi. Maandamano kadhaa yamefanyika kote nchini Australia mapema hii leo, kuwaunga mkono wakimbizi ambao bado wanaishi katika hali ya sintofahamu ndani ya vizuizi vya uhamiaji.

Wanasheria wanaomuwakilisha rais wa zamani wa Marekani, Donald Trump, wameapa kwamba mteja wao hatosaka tena makubaliano nje ya mahakama na badala yake yuko tayari kupambana dhidi ya mashitaka yote dhidi yake.

Mapigano mapya yamezuka Jumamosi asubuhi katika mji unaogombaniwa wa Las’anod nchini Somalia, si chini ya miezi miwili baada ya serikali ya Marekani kutaka kuondolewa kwa wanajeshi katika eneo hilo. Viongozi wa Sudan wameahirisha kutiwa saini kwa makubaliano yaliyopangwa kufanyika Jumamosi ili kurejesha kipindi kifupi cha mpito cha kidemokrasia, afisa mmoja amesema, huku hali ya kutoelewana ikiendelea kati ya makundi ya kijeshi.

Ombi la msamaha la bingwa wa zamani wa michezo ya Olimpiki kwa walemavu raia wa Afrika Kusini Oscar Pistorius, aliyefungwa jela mwaka 2016 kwa kumuua mpenzi wake Reeva Steenkamp limekataliwa. Haya ni kulingana na mamlaka za magereza Afrika Kusini na wakili wa familia ya Steenkamp.


Latest podcast episodes

Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Stream now