Taarifa ya Habari 2 Mei 2023

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Serikali ya shirikisho imedokeza uwezekano wakuongeza kiwango cha malipo ya Jobseeker katika bajeti ya wiki ijayo kwa wanao ipokea ambao wana zaidi ya miaka 55.


Idara ya elimu ya NSW inatarajiwa kutoa uhakika wa ajira kwa takriban walimu 1400, pamoja na wafanyakazi wasaidizi kama sehemu ya mpango wa kuajiri na kuhifadhi kwa shule. Mradi huo unalengo lakuhamisha idadi yawalimu wa muda elfu 10 pamoja na wafanyakazi wasaidizi elfu 6, katika mikataba yakudumu katika hatua ya kwanza, hatimae itafanya nafasi elfu 16 ziwe zakudumu kufukia 2024.

Waziri mkuu Anthony Albanese amethibitisha kuwa Mfalme Charles amepokea mwaliko kutembelea Australia. Hali hiyo imejiri siku chache baada yaku wasilishwa kwa kiapo cha umma kwa sherehe yakutawazwa, ambayo itawaalika raia wote wajamii yamadola kula kiapo cha utiifu kwa Mfalme na warithi wake.

Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula Duniani, WFP, Cindy McCain, amesema shirika hilo litaanza tena shughuli za utoaji misaada ya kiutu nchini Sudan, kufuatia mzozo nchini humo kuendelea kupambamoto.

Rais wa Kenya, William Ruto Jumatatu aliongoza sherehe za siku ya wafanyakazi duniani katika bustani ya Uhuru iliyoko katika jiji la Nairobi. Wakati wa maadhimisho hayo, Ruto alichukua nafasi kufafanua mikakati iliyowekwa na serikali yake katika kusaidia baadhi ya sekta zinazokua nchini nchini humo.

Nchini Tanzania wafanyakazi wameahidiwa kurejeshewa mfumo wa nyongeza ya mishahara wa kila mwaka ambayo ilikuwa umesitishwa miaka saba iliyopita na aliyekuwa raisi wa awamu ya tano John Pombe magufuli. Wafanyakazi hao pia wameitaka serikali kusimamia utekelezaji wa sheria za kazi ili kuleta usawa na haki katika maeneo ya kazi na kuepuka na tabia yakuongeza mishahara kama hisani



Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service
Taarifa ya Habari 2 Mei 2023 | SBS Swahili