Taarifa ya Habari 20 Machi 2022

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS Swahili

Wapiga kura waitimua serikali ya Kusini Australia katika uchaguzi, na serikali ya Queensland yataka usawa kutoka serikali ya madola katika ugavi wa msaada kwa waathiriwa wa mafuriko.


Serikali ya Queensland inaiomba serikali ya madola isawazishe msaada unao tolewa kwa waathiriwa wa mafuriko jimboni humo, na msaada unao tolewa kwa waathiriwa wa mafuriko wa New South Wales. Naibu kiongozi wa Queensland Stephen Miles ameomba serikali ya madola, iwekeze mfumo wa msaada wenye thamani ya $771 milioni, na isawazishe malipo ya janga kwa waathiriwa wao wa mafuriko.

Shane Warne ame agwa katika ibada ya mazishi ya faragha mjini Melbourne. Takriban idadi ya watu 80 walihudhuria ibada hiyo, katika klabu ya timu ya AFL ya St Kilda mapema hii leo Jumapili. Jeneza la Bw Warne lilizungushwa ndani ya uwanja huo mara moja baada ya ibada hiyo kama ishara ya heshima, familia yaki ikifuata kwa karibu. Ibada ya pili itafanywa ambako umma uta hudhuria katika uwanja maarufu wa Melbourne Cricket Ground, Melbourne, Victoria tarehe 30 Machi 2022.

Maelfu ya wakazi wa Kilimanjaro nchini Tanzania wamejitokeza kumlaki mwenyekiti wa chama cha upinzani- Chadema, Bwana Freeman Mbowe. Mbowe ameenda kwao Hai, kwa mara ya kwanza tangu atoke gerezani Machi 4, mwaka huu ambako alikaa kwa miezi minane akikabiliwa na tuhuma za ugaidi na uhujumu uchumi.

 

 


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service
Taarifa ya Habari 20 Machi 2022 | SBS Swahili