Watch FIFA World Cup 2026™

LIVE, FREE and EXCLUSIVE

Taarifa ya Habari 20 Novemba 2022

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Waziri Mkuu Anthony Albanese ame elezea imani yake kuwa vizuizi vya biashara kutoka China dhidi ya Australia vyenye thamani ya dola bilioni 20, vita anza kuondolewa baada ya mkutano wake na Rais Xi Jinping katika hoteli yamapumziko kisiwani Bali ambako mkutano wa G20 uliandaliwa.


Published

By Gode Migerano

Presented by Gode Migerano

Source: SBS



Share this with family and friends


Waziri Mkuu Anthony Albanese ame elezea imani yake kuwa vizuizi vya biashara kutoka China dhidi ya Australia vyenye thamani ya dola bilioni 20, vita anza kuondolewa baada ya mkutano wake na Rais Xi Jinping katika hoteli yamapumziko kisiwani Bali ambako mkutano wa G20 uliandaliwa.


Waziri Mkuu alisema miaka 50 yama husiano yakidiplomasia na Jamhuri yawatu wa China, kabla ya krismasi mwaka huu itakuwa fanikio mhimu, akidokeza kuwa inaweza kutana na kuondolewa kwa baadhi ya vizuizi vyakibiashara. Maadhimisho hayo yatafanyika rasmi Disemba 21.

Upinzani wa shirikisho ume iomba serikali isitishe muswada wayo wa mahusiano ya viwanda. Sussan Ley ame elezea madhara kwa biashara ndogo kama sababu ambayo serikali haistahili endelea na sheria zake za sehemu ya kazi, akisema biashara ndogo ndio uti wa mgongo wa uchumi wa Australia.

Rais wa zamani wa Kenya, Uhuru Kenyatta na Rais wa Rwanda Paul Kagame wamekubaliana juu ya haja ya waasi wa M23 kusitisha mapigano na kujiondoa katika maeneo waliyoteka mashariki mwa Congo, Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) imesema Ijumaa. Waasi wa M23 wamefanya mashambulizi kadhaa mashariki mwa Congo mwaka huu, ikiwa ni mara yao ya kwanza kurejea kwa kishindo tangu mwaka 2012, na kusababisha mapigano na jeshi ambayo yamesababisha maelfu ya raia kukimbia makazi yao tangu mwezi Machi. Machafuko hayo yalizua mivutano ya kidiplomasia kati ya Congo na nchi jirani ya Rwanda ambapo Congo inaishutumu nchi hiyo kwa kuliunga mkono kundi la M23. Rwanda imekanusha shutuma hizo.

Mataifa ya Afrika yanataka nchi tajiri kugharamia mabadiliko yahali ya hewa.

Mwaka huu pekee bara la Afrika limeshuhudia mafuriko mabaya sana huko Afrika Kusini na miaka kadhaa ya ukame mbaya huko Pembe ya Afrika. Mataifa ya Afrika katika mkutano wa COP27 yamesukuma sana kwa mataifa tajiri kulipa fidia ya hali ya hewa na kuchangia katika mfuko wa “hasara na uharibifu” .


Latest podcast episodes

Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Stream now