Taarifa ya Habari 21 2023

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili.jpg

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Upinzani wa shirikisho waukosoa mpango wa Waziri Mkuu, kufanya ziara China kabla ya vikwazo vyote vya kibiashara kuondolewa dhidi ya Australia.


Jimboni Qld polisi wame piga mwanaume mmoja risasi naku muuwa mchana wa leo katika eneo la kaskazini Brisbane. Polisi wamesema mwanaume huyo kutoka jamii yawa Australia wa kwanza, walipigwa risasi wakati walikuwa waki jibu wito kwa kesi ya vurugu ya nyumbani katika kitongoji cha Grange. Tukio hilo limejiri siku moja baada ya huduma za dharura kuitwa katika anwani hiyo, kwa sababu ya wasiwasi wa afya ya akili kuhusu mwanaume huyo.

Kiongozi wa chama cha Liberal cha Victoria, John Pesutto, amezomewa na wanao muunga mkono mbunge aliye furushwa kutoka chama hicho Moira Deeming. Katika kongamano la chama hicho mjini Bendigo, kundi dogo lililo kuwa na barakoa ya picha za sura ya Bi Deeming, lili beba mabango yaliyo muita Bw Pesutto mnyanyasaji pamoja naku paza sauti zao wakilalamika neno aibu.

Pande hasimu nchini Sudan, zimekubaliana kusitisha mapigano kwa siku saba kuanzia Jumatatu. Kwa mujibu wa wizara ya mambo ya ndani ya Marekani, pande hizo kwa mara ya kwanza zimefanya makubaliano na kutia sahihi zao. Taarifa iliyotolewa Jumamosi jioni imesema kwamba makubaliano hayo ya kuweka chini silaha yaliyofanyika mjini Jeddah Saudi Arabia, yanakusudia kuwapa watu wa Sudan nafasi ya kupata misaada ya kiutu.

Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe amewataka Watanzania kuacha kulalamika ugumu wa maisha na badala yake wachukue hatua kwa kuiondoa CCM madarakani.

Polisi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wametumia gesi kesi ya kutoa machozi ili kutawanya waandamanaji katika mji mkuu Kinshasa. Maandano hayo yaliitishwa na upinzani uliokuwa ukijimuhisha aliyekuwa waziri mkuu Matata Ponyo, Martin Fayulu, Moise Katumbi na Delly Sesanga wananuia kukemea gharama ya juu ya maisha ya kawaida, ukosefu wa usalama Mashariki mwa DRC na hali ya kutoweka wazi katika maandalizi ya uchaguzi uliopangwa kufanyika mwishoni mwa mwaka huu. Gavana wa mkoa wa Kinshasa, Gentini Ngobila pia amelaumu upinzani kutaka kuvuruga usalama wa umma.

Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service