Taarifa ya Habari 22 Disemba 2023

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Msaada wa kifedha wa ziada una tumwa kwa watu walio athiriwa kwa marufiko, wakati juhudi kubwa ya usafi ina anza katika ukanda wa Kaskazini Queensland.


Wazima moto wana wanakabiliana na mioto kadhaa ambayo imeharibu nyumba katika jimbo la Magharibi Australia, na wanakabiliana na siku nyingine ya mazingira magumu.

Upinzani wa shirikisho ume zindua mradi wakutoa uelewa kuhusu unyanyasaji wa nyumbani, kabla ya mwanzo wa msimu wa likizo. Kaimu kiongozi wa upinzani Sussan Ley pamoja na Seneta Kerrynne Liddle, wame waomba wa Australia watumie mitandao yakijamii kuchangia huduma zinazo patikana.

Wakati zoezi la kuhesabu kura likiwa linaendelea katika baadhi ya vituo vyakupigia kura nchini DRC, mjini Goma baadhi ya raia waliojitokeza tena kupiga kura wameshindwa kutekeleza haki yao na kurejea majumbani mwao.

Kuenea kwa mapigano kusini mashariki mwa Sudan kumeyalazimisha mashirika ya misaada ya kibinadamu kusitisha kwa muda operesheni zao kwenye baadhi ya maeneo, wakati UNICEF ikielezea wasi wasi wake kuhusu mamilioni ya watoto walio hatarini kutokana na ghasia zinazosambaa.

Rais wa Benin Patrice Talon siku ya Alhamisi amesema anataka kurejesha uhusiano kati ya nchi yake na nchi jirani ya Niger, ambayo hivi sasa inatawaliwa na viongozi wa kijeshi.


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service