Watch FIFA World Cup 2026™

LIVE, FREE and EXCLUSIVE

Taarifa ya Habari 22 Disemba 2023

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Msaada wa kifedha wa ziada una tumwa kwa watu walio athiriwa kwa marufiko, wakati juhudi kubwa ya usafi ina anza katika ukanda wa Kaskazini Queensland.


Published

Updated

By Gode Migerano

Presented by Gode Migerano

Source: SBS



Share this with family and friends


Msaada wa kifedha wa ziada una tumwa kwa watu walio athiriwa kwa marufiko, wakati juhudi kubwa ya usafi ina anza katika ukanda wa Kaskazini Queensland.


Wazima moto wana wanakabiliana na mioto kadhaa ambayo imeharibu nyumba katika jimbo la Magharibi Australia, na wanakabiliana na siku nyingine ya mazingira magumu.

Upinzani wa shirikisho ume zindua mradi wakutoa uelewa kuhusu unyanyasaji wa nyumbani, kabla ya mwanzo wa msimu wa likizo. Kaimu kiongozi wa upinzani Sussan Ley pamoja na Seneta Kerrynne Liddle, wame waomba wa Australia watumie mitandao yakijamii kuchangia huduma zinazo patikana.

Wakati zoezi la kuhesabu kura likiwa linaendelea katika baadhi ya vituo vyakupigia kura nchini DRC, mjini Goma baadhi ya raia waliojitokeza tena kupiga kura wameshindwa kutekeleza haki yao na kurejea majumbani mwao.

Kuenea kwa mapigano kusini mashariki mwa Sudan kumeyalazimisha mashirika ya misaada ya kibinadamu kusitisha kwa muda operesheni zao kwenye baadhi ya maeneo, wakati UNICEF ikielezea wasi wasi wake kuhusu mamilioni ya watoto walio hatarini kutokana na ghasia zinazosambaa.

Rais wa Benin Patrice Talon siku ya Alhamisi amesema anataka kurejesha uhusiano kati ya nchi yake na nchi jirani ya Niger, ambayo hivi sasa inatawaliwa na viongozi wa kijeshi.


Latest podcast episodes

Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Stream now