Taarifa ya Habari - 22 Machi 2022

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS Swahili

Serikali ya shirikisho yawaalika watalii katika maeneo ya Kaskazini Queensland, baada yakutangaza mfuko wa uwekezaji wakufufua sekta ya utalii katika maeneo hayo.


Kiongozi mpya wa jimbo la Kusini Australia Peter Malinauskas, ametangaza mageuzi kwa usimamizi wa UVIKO katika jimbo hilo. Ameongezea kuwa baraza lake la mawaziri, lita chukua nafasi ya kamati ya UVIKO-19 ya sasa.

Vikosi vya usalama vya Sudan vilimpiga risasi na kumuua kijana mmoja siku ya Jumatatu wakati wa msako mkali dhidi ya mapinduzi ya kijeshi ya mwaka jana madaktari walisema. Sudan imekumbwa na machafuko makubwa tangu mapinduzi ya kijeshi ya Oktoba yaliyoongozwa na mkuu wa jeshi Abdel Fattah al-Burhan ambayo yamesababisha maandamano ya mara kwa mara.

Serikali ya Kenya imesema kuwa inatarajia uchumi wake kuimarika kwa asilimia 6% mwaka huu , baada ya kunawiri kwa asilimia asilimia 9.9% katika robo ya tatu ya mwaka wa kifedha wa 2021 pamoja na kuongezeka kwa mapokeo ya fedha kutoka raia wake wanaoishi Ughaibuni.


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service