Taarifa ya habari 22 Novemba 2020

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS Swahili

Hatimae mpaka kati ya majimbo ya New South Wales na Victoria kufunguliwa, na kiongozi wa upinzani wa Magharibi Australia, ajiuzulu kabla ya uchaguzi jimboni humo.


Viongozi wa nchi zenye nguvu kiuchumi duniani wanafanya mkutano kwa njia ya video kujadili namna ya kupambana na corona na kuufufua uchumi wa ulimwengu. Kansela wa Ujerumani Angela Merkel amewahimiza viongozi wa nchi za G20 kuendelea kushirikiana katika vita dhidi ya virusi vya corona, akiuambia mkutano wa kilele unaofanyika kwa njia ya video kuwa mengi yanastahili kufanywa ili kulidhibiti janga hilo.

Mgombea urais wa Uganda na muimbaji mashuhuri Bobi Wine ameachiliwa kwa dhamani ijumaa wakati vifo vimefikia 37 vilivyo sababishwa na maandamano makubwa nchini humo. Mwanasiasa huyo ameachiliwa baada ya maafisa wa usalama kumfungulia mashtaka kwa madai ya kuwa kitendo chake cha kampeni kingeliweza kusambaza virusi vya corona.

Serikali ya Ethiopia imekataa juhudi za Umoja wa Afrika za upatanisho na kusema wanajeshi wake wamechukua udhibiti wa mji mwengine wakati jeshi la serikali linapoelekea katika mji mkuu wa mkoa wa kaskazini wa Tigray unaoshikiliwa na waasi. Mnamo siku ya Ijumaa, Umoja wa Afrika uliwateua marais wa zamani wa Msumbiji Joaquim Chissano, Ellen Johnsof Sirleaf wa Liberia na Kgalema Motlanthe wa Afrika Kusini kama wajumbe maalum katika mazungumzo ya upatanisho.


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service