Watch FIFA World Cup 2026™

LIVE, FREE and EXCLUSIVE

Taarifa ya Habari 22 Novemba 2022

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Waziri Mkuu na kiongozi wa New South Wales wametembelea mji wa Eugowra ambao uliathiriwa kwa mafuriko, kutangaza utoaji wa ruzuki ya ziada.


Published

By Gode Migerano

Presented by Gode Migerano

Source: SBS



Share this with family and friends


Waziri Mkuu na kiongozi wa New South Wales wametembelea mji wa Eugowra ambao uliathiriwa kwa mafuriko, kutangaza utoaji wa ruzuki ya ziada.


Huduma ya Jeshi la Polisi la Queensland [[QPS]], limekubali kufanya mageuzi kwa wafanyakazi baada ya ripoti iliyo toa ukosoaji mkali na lawama kwa viongozi kwa tamaduni iliyosambaa ya ubaguzi wa rangi na unyanyasaji wakijinsia katika jeshi hilo la Polisi.

Rais wa Kenya Dr William Ruto amesema kuwa wanajeshi wa jumuiya ya Afrika Mashariki "watahakikisha uwepo wa amani" mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, ambayo inakabiliwa na mashambulizi kutoka kundi la waasi wa M23. Katika mkutano na waandishi wa habari katika mji mkuu wa Kinshasa, Dr Ruto alisema wanajeshi hao wa kikanda "watatekeleza amani kwa wale wenye nia ya kuleta ukosefu wa utulivu." Wanajeshi wa Kenya, waliotumwa kama sehemu ya kikosi cha Jumuiya ya Afrika Mashariki, waliwasili hivi karibuni katika eneo hilo lenye machafuko.

Serikali ya kijeshi ya Mali Jumatatu ilipiga marufuku shughuli za mashirika yasiyo ya serikali yanayofadhiliwa au kuungwa mkono na Ufaransa, ikiwa ni pamoja na mashirika ya kibinadamu, huku kukiwa na mzozo unaozidi kuwa mbaya kati ya Paris na Bamako.

Waziri Mkuu wa muda wa taifa hilo la Afrika Magharibi Kanali Abdoulaye Maiga alihalalisha hatua hiyo katika taarifa yake kwenye mitandao ya kijamii, na kuitaja kuwa ni jibu kwa Ufaransa kusitisha misaada ya maendeleo kwa Mali hivi karibuni.


Latest podcast episodes

Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Stream now