Watch FIFA World Cup 2026™

LIVE, FREE and EXCLUSIVE

Taarifa ya habari 22 Septemba 2020

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS Swahili

Juhudi zakupunguza uzalishaji wa hewa chafu zapigwa jeki kwa uwekezaji wa dola milioni 18, na wakazi wa kaskazini New South Wales kupewa vibali vyakuingia Queensland.


Published

By Gode Migerano

Presented by Gode Migerano

Source: SBS



Share this with family and friends


Juhudi zakupunguza uzalishaji wa hewa chafu zapigwa jeki kwa uwekezaji wa dola milioni 18, na wakazi wa kaskazini New South Wales kupewa vibali vyakuingia Queensland.


Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres asikitishwa na ukosefu wa ushirikiano wa kimataifa katika kukabiliana na changamoto zinazoikabili dunia hi leo, alipokuwa anafungua mkutano wa viongozi kuadhimisha miaka 75 tangu kuundwa kwa umoja huo.

Jaji mkuu nchini Kenya David Maraga amemtaka rais Uhuru Kenyatta kulivunja bunge kwasababu halina wabunge wanawake wa kutosha. Katiba inasema kwamba jinsia moja haiwezi kudhibiti zaidi ya thuluthi mbili ya viti vya bunge. Hatahivyo wanawake wana viti vichache ikilinganishwa na viti 116 vinavyohitajika katika bunge hilo la wabunge 350.

Mali imewatangaza viongozi wa serikali mpya ya mpito, ambao utaweza kuendeleza mahusiano madhubuti na jeshi pamoja na uwepo wa shinikizo la kimataifa la kuteuliwa kwa kiongozi raia baada ya mapinduzi ya kijeshi. Katika taarifa yake ilioneshwa kwa njia ya video, kiongozi wa kijeshi Kanali, Assimi Goita amesema waziri wa zamani wa ulinzi Bah Ndaw, atakuwa rais wa serikali ya mpito wakati yeye mwenyewe atahudumu kama makamo wa rais.

 

 


Latest podcast episodes

Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Stream now