Taarifa ya Habari 23 Januari 2022

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS Swahili

Wanafunzi na walimu kupewa vipimo vya rapid antigen jimboni NSW, shule zitakapo funguliwa wiki ijayo, na hatimae tume ya usalama mtandaoni, yapewa mamlaka yakisheria kukabiliana na unyanyasaji wa mtandaoni.


Sheria mpya ya usalama mtandaoni ime anza kutumiwa leo, sheria hiyo inasema kwamba intanet haiko juu ya sheria. Waziri wa mawasiliano Paul Fletcher amesema sheria hiyo iliyopitishwa bungeni mwaka jana, ime anza kutumiwa kisheria leo hii Jumapili.

Rwanda na Uganda zimesema kwamba zimefanya mazungumzo ya kirafiki kuhusu kuboresha uhusiano baada ya Muhoozi Kainerugaba, mtoto wa rais wa Uganda Yoweri Museveni kukutana na rais wa Rwanda Paul Kagame mjini Kigali. Mazungumzo ya jana Jumamosi kati ya Kagame na Kainerugaba, jenerali anayedaiwa kuwa mrithi wa babake yamefanyika baada ya miaka mingi ya mvutano kati ya mataifa hayo mawili jirani.

Serikali ya Uingereza jana iliishtumu Urusi kwa kujaribu kuibadilisha serikali ya Ukraine na utawala unaoipendelea na kusema aliyekuwa mbunge wa Ukraine Yevheniy Murayev anazingatiwa kuwa mgombea anayetarajiwa. Serikali ya Uingereza ilitoa madai hayo kwa kuzingatia tathmini ya kijasusi bila ya kutoa ushahidi wa kuyathibitisha. Haya yanajiri huku kukiwa na vita vya maneno kati ya Urusi na mataifa ya Magharibi kuhusu hatua za Urusi dhidi ya Ukraine.


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service