Taarifa ya Habari 25 Aprili 2023

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili.jpg

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Wa Australia wameshiriki katika ibada za alfajiri za Anzac Day, pamoja na gwaride kuwaenzi walio hudumia nchi yao. Mwaka huu ni maadhimisho ya miaka 108 ya kampeni ya Gallipoli, katika vita vya kwanza vya dunia nchini Turkiye.


Serikali ya shirikisho ita anzisha sajili mpya kwa ulaghai wa ujumbe wa simu za rununu, wakati idadi kubwa yawa Australia wanaendelea kuwa waathiriwa wa ulaghai mtandaoni.
47% yawa Australia wameripoti kuwa wamepokea jumbe fupi za sami kutoka kwa walaghai, katika mwaka uliopita wakati wa Australia walipoteza zaidi ya bilioni 3 za dola kupitia ulaghai katika mwaka wa 2022. Dola milioni 10 zitawekezwa, kuzindua sajili hiyo mpya katika bajeti ya shirikisho mwezi ujao.

Majenerali wanaopingana nchini Sudan wamekubali kusitisha mapigano kwa siku tatu kuanzia usiku wa kuamkia hii leo Jumanne licha ya makubaliano ya hapo awali kuvunjika ndani ya muda mfupi. Wakati ambapo serikali za kigeni zikiendelea na zoezi la kuwahamisha mamia ya wanadiplomasia wao pamoja na raia wao kuwapeleka mahala salama, Wasudan wanahangaika kutafuta njia za kuepuka machafuko hayo, wakihofia kwamba pande mbili za jeshi zinazopingana nchini humo zitazidisha vita vyao vya kuwania madaraka mara baada ya nchi za kigeni zitakapomilisha shughuli za kuwaondoa raia wao.

Idadi ya waliofariki katika tukio lililohusisha dhehebu la Kenya lililoamuru waumini wake kukaa na njaa hadi kufa iliongezeka na kufikia 73 Jumatatu, vyanzo vya polisi vimeiambia AFP. Wanaofanya uchunguzi walifukua maiti zaidi kutoka kwenye makaburi ya watu wengi katika msitu karibu na pwani. Uchunguzi ulianzishwa dhidi ya kanisa la Good News International Church na kiongozi wake Paul Mackenzie Nthenge ambaye alitajwa katika hati za mahakama, ambaye alihubiri kuwa kifo cha njaa kitawafikisha waumini kwa Mungu.


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service