Taarifa ya Habari 25 Juni 2023

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Waziri wa wa fedha Julie Collins ametetea uwekezaji wa serikali wenye thamani ya bilioni 10 kupitia mradi wa Housing Australia Future Fund, wakati vyama vya Greens na Mseto viki endelea kuzuia muswada huo kupita bungeni.


Serikali ya New South Wales imesema itaharakisha jaribio la kuwaruhusu madereva kupunguza alama moja ya adhabu, kama wameonesha rekodi nzuri yakuendesha gari.

Utafiti mpya unatabiri kuwa idadi yawatu wazima wanao ishi na ugonjwa wa kisukari kote duniani ita ongezeka mara mbili kufikia 2050. Utafiti huo unalaumu kuongezeka kwa kasi kwa viwango vya fetma, na kuongezeka kwa uhaba wa usawa katika afya kwa watu wazima bilioni 1.3 ambao watakuwa na kisukari ndani ya miongo ijayo.

Mamluki wa kampuni binafsi ya kijeshi ya Wagner wameanza leo kurejea kwenye kambi zao baada ya kiongozi wao Yevgeny Prigozhin kukubali kwenda uhamishoni nchini Belarus.

Umoja wa Mataifa, Jumamosi umetoa mwito wa kuchukuliwa hatua za haraka kukomesha mauaji ya kiholela ya watu wanaokimbia El Geneina, mji mkuu wa jimbo la Darfur Magharibi, na wanamgambo wa kiarabu wakisaidiwa na wanajeshi wa jeshi la taifa.


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service
Taarifa ya Habari 25 Juni 2023 | SBS Swahili