Taarifa ya habari 26 Januari 2021

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS Swahili

Mtetezi wa wahamiaji miongoni mwa washindi wa tuzo zawa Australia wa mwaka na, zaidi ya idadi yawahamiaji elfu 12, wapokea uraia wa Australia katika sherehe kote nchini.


Baraza la Wawakilishi la Bunge la Marekani limewasilisha hati ya mashtaka mbele ya Baraza la Seneti dhidi ya rais wa zamani Donald Trump na kufungua njia ya kuanza kwa shauri la pili la kihistoria.

Mahakama moja Uganda imeamuru vikosi vya usalama kuacha kuzingira nyumba ya kiongozi wa upinzani Robert Kyagulani anayejulikana pia kwa jina lake la usanii Bobi Wine. Wine alikuwa anazuiliwa nyumbani kwake tangu uchaguzi wa rais katikati ya mwezi na kumesababisha shinikizo la kimataifa aachiliwe, wakili wake alisema Jumatatu.

Gavana wa Kivu Kaskazini anawasihi raia kushirikiana na jeshi kusitisha uasi. Amesema juhudi za jeshi pekee hazitoshi, ikiwa wananchi hawatatoa mchango kamili katika kufanikisha suala hilo.


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service