Taarifa ya Habari 26 Oktoba 2021

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS Swahili

Serikali ya shirikisho yajitetea baada yakushtumiwa kwa uzembe, kwa kufanyia kazi swala lakupunguza uzalishaji wa hewa chafu nchini.


Queensland yajiandaa kuanza kuwapokea tena wanafunzi wakimataifa punde baada yakukamilika ujenzi wa makazi ya karantini mjini Toowoomba, na Kusini Australia kufungua mipaka yake yote kwa watu ambao wamepata chanjo kamili za Uviko-19.

Umati wa watu umefanya maandamano hadi jana usiku nchini Sudan kupinga mapinduzi ya kijeshi, huku vurugu zikiugubika mji mkuu Khartoum baada ya wanajeshi kuwafyatulia risasi waandamanaji na kudaiwa kuwauwa watu watatu.

Kampuni ya dawa ya Aspen ya Afrika kusini yajipanga kutengeneza chanjo zaidi za COVID-19. Aspen inakusudia kuongeza uwezo wake wa utengenezaji wa chanjo ya COVID-19 hadi dozi bilioni 1.3 kwa mwaka ifikapo Februari mwaka 2024 kutoka kwenye pato la sasa la dozi karibu milioni 250 kwa mujibu wa mkurugenzi mtendaji wa kampuni hiyo, Stephen Saad


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service