Taarifa ya Habari 27 Septemba 2022

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Asilimia 95 ya familia zenye watoto nchini Australia, kufaidi kupitia mageuzi ya serikali ya shirikisho kwa gharama ya huduma ya malezi ya watoto.


Serikali ya Labor imezindua kampeni yake yakuanzisha tume ya shirikisho yakukabiliana na ufisadi. Serikali imesema ita ahidi uwekezaji wa dola milioni $262 kwa muda wa miaka minne, kuhakikisha tume hiyo inarasilimali yakutosha kudumisha uadilifu katika maisha ya umma.

Akaunti inayo dai kuhusika na udukuzi wa data za Optus, imeomba radhi nakusema imeondoa tisho lake lakuteka nyara data zawatumiaji. Akaunti hiyo ya mtandaoni iliyo toa tisho hizo, inaaminika kuwa ni halali na wataalam wa usalama wa mtandaoni ila, bado haija thibitishwa na Optus pamoja na Jeshi la polisi la shirikisho. Akaunti hiyo mwanzoni ilitishia kuchapisha data zaidi za wateja, kama Optus haita ilipa $1.5 milioni ((AUD)).

Idadi ya watu waloambukizwa na ugonjwa wa Ebola inazidi kuongezeka nchini Uganda. Wizara ya afya inasema kumekuwa na watu 34 wanaodhaniwa wameambukizwa na virusi hivyo vya hatari. Inaamini kwamba watu 21 wamefariki kutokana na Ebola. Nchi jirani zimesema ziko katika hali ya tahadhari kubwa.

Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service
Taarifa ya Habari 27 Septemba 2022 | SBS Swahili