Taarifa ya Habari 28 Mei 2023

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Wiki ya Maridhiano ya Kitaifa imeanza kote nchini na wanaharakati wamesema, tukio la mwaka huu ni mhimu haswa kwa sababu ya kura ya maoni ijayo kwa sauti yawa Australia wa kwanza bungeni.


Chama cha Labor kimetoa rasimu ya mkakati wakitaifa kwa sekta za huduma ya Australia, kikiapa kukarabati sekta ya huduma yawazee, walemavu, maveterani na mfumo elimu yamapema ya watoto. Mkakati wa rasimu hiyo unasema kuona viwango vya juu vya wato wanao ondoka katika sekta hizo kwa sababu, ya malipo duni na kuto tambuliwa kwa kazi hizo, mwendelezo mdogo wa taaluma, viwango vya juu vya majukumu na wakati mwingine mazingira yasiyo salama ya kazi.

Marekani na Saudi Arabia zimetoa mwito kwa pande hasimu nchini Sudan kuongeza muda wa kusimamisha mapigano utakaofika kikomo kesho Jumatatu. Katika taarifa ya pamoja iliyotolewa mapema leo, Washington na Riyadh zimesema kurefushwa kwa muda wa kuweka chini silaha kutawezesha utoaji wa misaada ya kiutu ya haraka inayohitajika kwa watu wa Sudan.

Rais wa Uganda Yoweri Museveni amesema kuna wanajeshi waliopoteza maisha katika shambulio lililofanywa na kundi la Al Shabaab, dhidi ya kambi ya jeshi la walinda amani wa Umoja wa Afrika kutoka Uganda nchini Somalia. Kwenye taarifa iliyonukuliwa na shirika la habari la Reuters, Museveni hakutaja idadi ya wanajeshi waliojeruhiwa au kuuwawa.






Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service