Taarifa ya Habari 3 Machi 2022

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS Swahili

Waziri Mkuu aendelea kukanusha madai kuwa alitumia kauli zaubaguzi wa rangi katika kampeni za mchujo wa wagombea wa chama cha Liberal alipochaguliwa mara ya kwanza kuwania ubunge.


Mweka hazina kivuli Jim Chalmers amesema hapatakuwa ongezeko ya kodi kama chama cha Labor kinashinda uchaguzi wa Mei, isipokuwa mpango wake ambao umewekwa wazi kufanya kazi na nchi zingine zinazo lenga mashirika yakimataifa.

Kundi la waasi la M23 linaloshutumiwa kwa kutekeleza mashambulizi mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo limetangaza kusitisha mapigano, baada ya siku kadhaa za makabiliano makali na jeshi la kitaifa la DRC, msemaji wake amesema kupitia taarifa. Kundi hilo limesema linataka fanya mazungumzo na serikali na kwamba limewaondoa wapiganaji wake katika eneo la mapigano, ili kuepusha makabiliano mapya na jeshi la Kongo.

Shirikisho la kimataifa la Msalaba Mwekundu, limesema kwamba Juhudi za kufikisha misaada ya dawa katika eneo la Tigray, lililokumbwa na vita, zimeshindikana. Hii ni licha ya sitisho la mapigano kati ya serikali na majeshi ya Tigray, ya kuruhusu misaada kuingia sehemu hiyo.

 


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service
Taarifa ya Habari 3 Machi 2022 | SBS Swahili