Taarifa ya Habari 3 Mei 2022

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS Swahili

Waziri Mkuu ajiweka mbali na ongezeko ya riba, hata hivyo upinzani wamtungia kidole cha lawama.


Waziri wa elimu wa NSW amehamasisha chama cha walimu cha jimbo hilo, kifute mgomo wa kesho akiahidi kuwa bajeti ya mwezi ujao utashughulikia mishara ya sekta ya umma. Ila rais wa chama cha walimu cha NSW Angelo Gavrielatos, amesema mgomo utafanyika ulivyo ratibiwa walimu wanapo omba nyongeza kwa mshahara wao kutoka 5% hadi 7.5%.

Mamlaka ya magereza nchini Morocco imekuwa ikitoa mafunzo ya kutokomeza ugaidi tangu mwaka 2017 kwa wapiganaji wa zamani wa kundi la Islamic State (IS) na wengine waliopatikana na hatia ya makosa ya ugaidi. Program ya tisa ya kundi la wahitimu lilimaliza masomo wiki iliyopita. Vyombo vya habari vili alikwa kushuhudia sherehe zao za kuhitimu katika gereza la Sale karibu na mji mkuu Rabat. Kuhitimu kutoka kwenye mpango huo hakufanyi wafungwa wastahiki moja kwa moja kuachiliwa mapema lakini kunaongeza fursa zao za kupata msamaha au kupunguziwa adhabu.

Magenge yenye silaha ambayo yamewateka nyara maelfu ya abiria katika shambulizi la kwenye treni huko kaskazini mwa Nigeria yanatumia raia kama ngao ya kibinadamu na hivyo kufanya iwe vigumu kwa jeshi kutekeleza kazi ya uokoaji Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari alisema Jumatatu. Shirika la reli la serikali ya Nigeria lilisema mwezi uliopita kuwa watu 168 walipotea kufuatia shambulizi la Machi 28.

 


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service