Taarifa ya habari 3 Novemba 2020

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS Swahili

Wanaume kukabiliwa na changamoto zaidi zaukosefu wa ajira kwa sababu ya COVID-19, aonya mbunge wa chama cha Labor


Rais wa Marekani Donald Trump na mpinzani wake wa Democratic Joe Biden wametumia saa zao za mwisho za mbio za kuelekea Ikulu katika majimbo magumu. Bwana Biden alifanya kampeni Pennsylvania na Ohio, wakati Bwana Trump akiwa Winsconsin, Michigan, North Carolina na Pennsylvania.

Mwanasiasa wa upinzani nchini Tanzania, Tundu Lissu, alikamatwa kwa muda na kuachiliwa Jumatatu baada ya polisi kusema wamefanikiwa kuzima maandamano yaliyokuwa yameitishwa na waupinzani kupinga matokeo ya uchaguzi mkuu wa wiki iliyopita. Wanasiasa kadhaa wa upinzani wamekamatwa wakati na baada ya matokeo ya uchaguzi huo kutangazwa.

Wakili mmoja wa Kenya amejisalimisha kwa viongozi wa Uholanzi ili kukabiliana na mashtaka dhidi yake kwenye mahakama ya kimataifa ya uhalifu (ICC). Wakili huyo anadaiwa kuwahonga mashahidi katika kesi dhidi makamu rais wa Kenya William Ruto katika mahakama hiyo.


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service