Watch FIFA World Cup 2026™

LIVE, FREE and EXCLUSIVE

Taarifa ya habari 3 Novemba 2020

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS Swahili

Wanaume kukabiliwa na changamoto zaidi zaukosefu wa ajira kwa sababu ya COVID-19, aonya mbunge wa chama cha Labor


Published

By Gode Migerano

Presented by Gode Migerano

Source: SBS



Share this with family and friends


Wanaume kukabiliwa na changamoto zaidi zaukosefu wa ajira kwa sababu ya COVID-19, aonya mbunge wa chama cha Labor


Rais wa Marekani Donald Trump na mpinzani wake wa Democratic Joe Biden wametumia saa zao za mwisho za mbio za kuelekea Ikulu katika majimbo magumu. Bwana Biden alifanya kampeni Pennsylvania na Ohio, wakati Bwana Trump akiwa Winsconsin, Michigan, North Carolina na Pennsylvania.

Mwanasiasa wa upinzani nchini Tanzania, Tundu Lissu, alikamatwa kwa muda na kuachiliwa Jumatatu baada ya polisi kusema wamefanikiwa kuzima maandamano yaliyokuwa yameitishwa na waupinzani kupinga matokeo ya uchaguzi mkuu wa wiki iliyopita. Wanasiasa kadhaa wa upinzani wamekamatwa wakati na baada ya matokeo ya uchaguzi huo kutangazwa.

Wakili mmoja wa Kenya amejisalimisha kwa viongozi wa Uholanzi ili kukabiliana na mashtaka dhidi yake kwenye mahakama ya kimataifa ya uhalifu (ICC). Wakili huyo anadaiwa kuwahonga mashahidi katika kesi dhidi makamu rais wa Kenya William Ruto katika mahakama hiyo.


Latest podcast episodes

Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Stream now