Taarifa ya Habari 30 Julai 2023

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Muswada wa nyongeza ya malipo ya Jobseeker, unatarajiwa kuwasilishwa bungeni vikao vitakapo anza tena kesho Jumatatu 31 Julai 2023.


Waziri wa huduma za jamii Amanda Rishworth, ametangaza tayari kuwa mafao hayo yakutokuwa na ajira yata ongezwa kwa dola 40 kila wiki mbili kuanzia Septemba.

Uchunguzi umeanza kwa kilicho sababisha ajali ya helikopta ya jeshi, katika visiwa vya Whitsunday jimboni Queensland. Timu ya wachunguzi wa ajali hiyo, ime wasili jimboni Qld kuanza uchunguzi wakati vikosi vyakutafuta nakuokoa vina endelea kupekua eneo hilo kwa mabaki ya helikopta hiyo pamoja na walio kuwa ndani yake.

Wiki ya watu walio potea ime anza kwa juhudi zaku toa uelewa wa watu ambao wame potea kwa muda mrefu na, kumulika kiwewe ambacho wapendwa wao wanao acha nyuma hupitia. Hisia za matumaini, kutoweza kufanya chochote ambacho wapendwa huhisi, huzingatiwa kuwa moja ya aina mbaya ya viwewe na dhidi wanayo pitia wakati kuna huduma chache sana za misaada.

Kumekuwa na maoni mchanganyiko miongoni mwa Wasudan kuhusiana na hatma ya mapigano yanayoendelea kati ya majenerali wawili waliohasimiana. Huku baadhi yao wakiwa na matumaini huenda mapigano yakamalizika na wengine wakiwa wamepoteza matumani ya kurejea kwa amani katika taifa hilo la Afrika.

Mahasimu wakuu wakisiasa nchini Kenya hatimae wakubali kufanya mazungumzo, mirengo ya Kenya Kwanza na Azimio One Kenya ilitoa taarifa kwa umma kuhusu maamuzi waliyo fikia.

Rais wa Burundi Evariste Ndayishimiye, Ijumaa amewasili kwenye mji mkuu wa jimbo la Sichuan, wa Chengdu, kusini-magharibi mwa China, ili kuhudhuria hafla ya ufunguzi wa michezo ya 31, ya shirikisho la michezo ya vyuo vikuu vya kimataifa, FISU, pamoja na kutembelea China.

Morrocco timu ya pili kutoka Afrika kushinda mechi katika kombe la dunia la FIFA, wenyeji NewZealand watupwa nje na hatma ya Australia i mikononi mwake kesho usiku.


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service