Watch FIFA World Cup 2026™

LIVE, FREE and EXCLUSIVE

Taarifa ya Habari 30 Mei 2023

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Kampuni moja iliyopewa kandarasi imesimamishwa kushiriki katika miradi yote kubwa ya reli, baada yaku kumbwa kwa kasha ya utapeli jimboni Victoria.


Published

By Gode Migerano

Presented by Gode Migerano

Source: SBS



Share this with family and friends


Kampuni moja iliyopewa kandarasi imesimamishwa kushiriki katika miradi yote kubwa ya reli, baada yaku kumbwa kwa kasha ya utapeli jimboni Victoria.


Wafanyakazi wanao wahudumia wagonjwa katika wakati wa dharura jimboni NSW, wauguzi pamoja na wafanyakazi wengine wa huduma ya afya, wana ongeza hatua zao zakuomba nyongeza kwa mshahara wao, baada ya serikali ya Labor kufeli kutimiza ahadi yakuongeza mishahara hiyo miezi mbili baada yakuingia madarakani.

Waziri Mkuu Anthony Albanese amesema kuwa wa Australia wanao pinga sauti yawa Australia wakwanza bungeni si wabaguzi wa rangi. Kauli hiyo inafuata shutma za kiongozi wa upinzani Peter Dutton dhidi ya waziri mkuu, kuhusu matamshi ya matusi kuhusu mjadala wa the Voice.

Rais wa Marekani Joe Biden Jumatatu ameishutumu sheria mpya ya Uganda inayopinga mapenzi ya jinsia moja na kusema kuwa inakiuka haki za binadamu, na inahatarisha maendeleo ya uchumi wa nchi hiyo iliyoko mashariki mwa bara la Afrika.

Kenya itatia saini mkataba wa biashara na Urusi unaolenga kuimarisha ushirikiano wa kibiashara, ofisi ya Rais William Ruto ilisema siku ya Jumatatu, baada ya kumkaribisha Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi, Sergei Lavrov jijini Nairobi.


Latest podcast episodes

Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Stream now