Taarifa ya Habari 30 Mei 2023

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Kampuni moja iliyopewa kandarasi imesimamishwa kushiriki katika miradi yote kubwa ya reli, baada yaku kumbwa kwa kasha ya utapeli jimboni Victoria.


Wafanyakazi wanao wahudumia wagonjwa katika wakati wa dharura jimboni NSW, wauguzi pamoja na wafanyakazi wengine wa huduma ya afya, wana ongeza hatua zao zakuomba nyongeza kwa mshahara wao, baada ya serikali ya Labor kufeli kutimiza ahadi yakuongeza mishahara hiyo miezi mbili baada yakuingia madarakani.

Waziri Mkuu Anthony Albanese amesema kuwa wa Australia wanao pinga sauti yawa Australia wakwanza bungeni si wabaguzi wa rangi. Kauli hiyo inafuata shutma za kiongozi wa upinzani Peter Dutton dhidi ya waziri mkuu, kuhusu matamshi ya matusi kuhusu mjadala wa the Voice.

Rais wa Marekani Joe Biden Jumatatu ameishutumu sheria mpya ya Uganda inayopinga mapenzi ya jinsia moja na kusema kuwa inakiuka haki za binadamu, na inahatarisha maendeleo ya uchumi wa nchi hiyo iliyoko mashariki mwa bara la Afrika.

Kenya itatia saini mkataba wa biashara na Urusi unaolenga kuimarisha ushirikiano wa kibiashara, ofisi ya Rais William Ruto ilisema siku ya Jumatatu, baada ya kumkaribisha Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi, Sergei Lavrov jijini Nairobi.


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service