Taarifa ya habari 31 Januari 2021

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS Swahili

Australia kutowekwa kwenye orodha ya nchi, ambazo zitawekewa masharti ya udhibiti wa mauzo ya chanjo ya COVID-19.


Wanasiasa watarejea bungeni kesho, uponaji wa Australia kutoka janga la COVID-19 ikiwa kipaumbele kwenye ajenda. Wanasiasa hao wanarejea bungeni wakati serikali imethibitisha mipango yake yaku sitisha, marupurupu ya JobKeeper kuanzia Machi, wakati idadi yawa Australia milioni 2.1 hawapokei tena malipo hayo.

Wabunge kadhaa wa Marekani hivi karibuni wamepokea vitisho kwa maisha yao, wakati Spika wa Baraza la Wawakilishi Nancy Pelosi akitaka usalama uimarishwe katika Bunge la Marekani na kudai kuwa kuna hatari inayokuja siyo tu kutoka uraiani lakini kutoka kwa “adui wa ndani” ya Bunge lenyewe.

Wasiwasi unaongezeka nchini Tanzania kuhusu kuenea kwa maambukizi ya ugonjwa wa corona licha ya matamshi ya serikali kukanusha kwamba ugonjwa huo haupo nchini humo. Kwa karibu mwaka mzima Tanzania imedai hakuna corona nchini humo, na kuwa nchi pekee Afrika Mashariki ambayo haina masharti rasmi ya kujikinga na ugonjwa huo.


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service