Watch FIFA World Cup 2026™

LIVE, FREE and EXCLUSIVE

Taarifa ya Habari 31 Oktoba 2023

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Waziri Bill Shorten amesema taarifa ya pamoja iliyo tiwa saini na mawaziri wakuu sita wa zamani wa Australia, kuhusu vita vya Gaza, kimsingi ina mulika msimamo wa serikali ya shirikisho.


Published

Updated

By Gode Migerano

Presented by Gode Migerano

Source: SBS



Share this with family and friends


Waziri Bill Shorten amesema taarifa ya pamoja iliyo tiwa saini na mawaziri wakuu sita wa zamani wa Australia, kuhusu vita vya Gaza, kimsingi ina mulika msimamo wa serikali ya shirikisho.


Wafanyakazi wa muda ambao hawataki hamia katika mikataba yakudumu, hawata lazimishwa kuwa na mikataba hiyo baada ya serikali kukubali kurekebisha muswada wa mageuzi ya kazini. Hali hii imejiri wakati baadhi ya sekta, zinazo jumuisha migahawa na maduka ya rejareja, ilizua wasiwasi kuwa wafanyakazi wa muda wata lazimishwa katika mikataba ya kufanya kazi kwa masaa mengi, hali ambayo inge ondoa mafao yao pamoja na faida zingine.

Ziara ya mfalme Charles wa Uingereza imezua hisia tofauti miongoni mwa Wakenya, ambao baadhi yao wanaiona ziara hiyo kuwa fursa nzuri ya kuimarisha uhusiano wa muda mrefu kati ya nchi hizo mbili. Huku baadhi ya Wakenya wakijiandaa kufanya maandamano kudai fidia kutokana na dhuluma zilizofanywa na wanajeshi wa Uingereza katika kambi ya jeshi ya Nanyuki. Lakini baadhi ya Wakenya wamesema watafanya maandamano siku ya Jumanne kupinga ukatili waliofanywa na baadhi ya wanajeshi katika kambi ya Nanyuki pamoja na kuulalamikia utawala wa kikoloni. Mfalme Charles anaanza ziara yake ya kwanza kama mfalme katika taifa la Jumuiya ya Madola, ambapo maoni yoyote atakayotoa juu ya historia ya ukoloni wa Uingereza yatafuatiliwa kwa karibu.

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu ametupilia mbali miito ya usitishwaji mapigano dhidi ya kundi la Hamas katika Ukanda wa Gaza. Netanyahu amesema wito wa usitishwaji mapigano ni sawa na kuitaka Israel kujisalimisha kwa kundi la Hamas na kuafiki ugaidi na ukatili. Amesema hilo haliwezekani na kunukuu Biblia kwamba kuna wakati wa amani na wakati wa vita, na kwamba sasa ni wakati wa vita ili kuandaa mustakabali wa pamoja.


Latest podcast episodes

Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Stream now