Taarifa ya Habari 5 Septemba 2021

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili Source: SBS Swahili

Jimbo la New South Wales limerekodi idadi ya kesi 1485 ya maambukizi mapya ya Covid-19 ndani ya jamii.


Kumekuwa vifo vingine vitatu, vyote vikiwa katika maeneo ya Magharibi na kusini magharibi Sydney. Watu hao ni watu wawili ambao walikuwa hawaja chanjwa na walikuwa na magonjwa mbali mbali, na mwingine alikuwa amepokea dozi moja tu ya chanjo. 40% ya wakaaji wote wanao stahiki kwa sasa wamepokea chanjo kamili, wakati 73% yawakaaji jimboni humo wame pokea dozi moja ya chanjo.

Vizuizi jimboni Victoria vinaweza regezwa mapema kuliko ilivyo ratibiwa, wakati 60% ya wakaaji wa Victoria wanapokea dozi yao ya kwanza ya chanjo. Jimbo hilo lilirekodi kesi mpya 183 za coronavirus na 82, ambazo hazija ungwa na milipuko inayo julikana. Mzunguko wa kilomita 5 uta ongezwa, wakati wa ziada wa mazoezi utaruhusiwa na kufunguliwa tena kwa vifaa vya kufanyia mazoezi nje, punde jimbo hilo litakapo fikia 70% ya dozi ya kwanza ya chanjo.

Polisi Tanzania imesema Ijumaa walikuwa wanachunguza madai dhidi ya baadhi ya maafisa wa polisi kuhusika na ubakaji na udhalilishaji wa kingono wa wanawake kadhaa katika vilabu vya usiku. Hatua hii ni kufuatia kusambaa madai hayo ambayo yalisababisha malalamiko na wito wa kuchukuliwa hatua za haraka. Shutuma hizo zimetolewa wakati wa mkutano wa hadhara na kamishna wa polisi wa wilaya ya Handeni, katika mkoa wa Tanga wiki hii.

 


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service