Taarifa ya Habari 7 Agosti 2022

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Ziara ya spika wa bunge ya Marekani, yazua tumbojoto kwa mahusiano kati ya Australia na China.


Serikali ya shirikisho imesema mfumo wakutoa alama za ubora kwa makaazi ya huduma ya wazee, unatarajiwa kutumiwa kufikia mwisho wa mwaka huu. Mfumo huu utatoa alama kwa makaazi kwa maswala tofauti ya malezi na huduma, kuruhusu familia zichague makaazi yanayo tosheleza mahitaji yao.

Watu wenye silaha wamewaua watu sita, wakiwemo W]wahindi wawili, katika jimbo la Kogi nchini Nigeria, polisi walisema Jumamosi, huku eneo hilo likikumbwa na ghasia za wanajihadi na magenge.

Wagombea urais nchini Kenya, kiongozi wa chama cha ODM Raila Odinga na Naibu wa Rais William Ruto, Jumamosi walihutubia mikutano yao ya mwisho ya kampeni mjini Nairobi kwelekea kwa uchaguzi mkuu Jumanne wiki ijayo. Kwa mujibu wa kanuni za uchaguzi, Jumamosi ilikuwa siku ya mwisho kwa wagombea, vyama na miungano ya kisisasa kufanya mikutano ya kampeni kote nchini.


Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service