Watch FIFA World Cup 2026™

LIVE, FREE and EXCLUSIVE

Taarifa ya Habari 9 Agosti 2022

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili.jpg

Bango la taarifa ya habari la SBS Kiswahili

Wiki mbili baada yakujiuzulu, aliyekuwa naibu kiongozi wa New South Wales aendelea kukabiliwa kwa maswali, kuhusu alivyo teuliwa kuwa mjumbe wa biashara wa jimbo la NSWmjini New York


Published

By Gode Migerano

Presented by Gode Migerano

Source: SBS


Share this with family and friends


Wiki mbili baada yakujiuzulu, aliyekuwa naibu kiongozi wa New South Wales aendelea kukabiliwa kwa maswali, kuhusu alivyo teuliwa kuwa mjumbe wa biashara wa jimbo la NSWmjini New York


Chama cha The Greens cha shirikisho chataka swala la mkataba na jamii yawa Australia wakwanza, lijumuishwe kama sehemu yakutoa sauti yawa Australia wa kwanza bungeni.

Mamilioni ya Wakenya wameanza kumiminika katika vituo vya kupigia kura mapema leo kumchagua rais mpya, bunge na viongozi wengine. Kiti cha urais kinawaniwa na wagombea wanne ambao ni mwanasiasa mkongwe Raila Odinga, Makamu Rais William Ruto, George Wajackoyah na David Mwaure. Kura za maoni zimetabiri ushindani mkali kati ya Odinga na Ruto. Jumla ya wapiga kura milioni 22 wamejiandikisha kushiriki uchaguzi wa leo utakaohitimisha utawala wa rais Uhuru Kenyatta.

Rais wa Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo Felix Tshisekedi anatarajiwa kujadili mvutano ulioko kati ya nchi yake na Rwanda wakati wa ziara ya waziri wa mambo ya nje wa Marekani Antony Blinken mjini Kinshasa leo Jumanne, ofisi ya rais ilisema Jumatatu. Mvutano ulizuka tena kati ya DRC na jirani yake Rwanda, serikali ya DRC ikiishtumu Rwanda kuunga mkono waasi wa M23, tuhuma ambazo zinakanushwa na serikali ya Rwanda.


Latest podcast episodes

Follow SBS Swahili

Download our apps

Listen to our podcasts

Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service

Stream now