Michuano ya kombe ya Afrika jijini Sydney, ilianza kwa kasi na vichapo katika viwanja vya mazoezi vya Western Sydney Wanderers.
Afrika ya kati na mashariki ina wakilishwa na Tanzania, na D R Congo katika michuano hiyo.
Katika mechi ya kwanza ya michuano hiyo, vijana wa Tanzania walikutana na vijana wa Sudan katika dimba hilo, na nyavu za timu hizo mbili, hazikuweza hifadhi siri za yaliyo jiri katika mechi hiyo.
Mwanaspoti wetu Frank Mtao, alihudhuria mechi hiyo nakuzungumza na mashabiki pamoja na mwalimu msaidizi wa Tanzania baada ya mechi hiyo. Bofya hapo juu kwa taarifa kamili.
Share






