Shirika la ANSA, huandaa michuano ya soka kwa niaba ya jamii zaki Afrika mjini Sydney, New South Wales.
Katika miaka ya kwanza ya michuano hiyo, Tanzania ilikuwa timu yaku ogopwa ila ukali wao ulififia kila msimu.
Hata hivyo, vijana wa Tanzania wamerejeshea timu yao heshima tena, baada ya miaka kadhaa yakufeli kuondoka katika kundi lao nakutinga robo fainali kwa mara ya kwanza baada ya zaidi ya miaka minane.

Idhaa ya Kiswahili ya SBS, ilizungumza na viongozi wa jamii na timu hiyo, kuhusu hatua hiyo yakihistoria kwa timu ya Tanzania katika michuano hiyo.
Share





