Kugawa au kutogawa: Mjadala wa marejesho ya makato ya kodi wa anza bungeni

Mweka hazina kivuli Chris Bowen akizungumza na waandishi wa habari ndani ya bunge la taifa mjini Canberra, Australia

Mweka hazina kivuli Chris Bowen akizungumza na waandishi wa habari ndani ya bunge la taifa mjini Canberra, Australia Jumatatu, 18 Juni 2018 Source: AAP

Waziri mkuu Malcolm Turnbull ame ihamasisha seneti ipitishe mpango wa serikali wa makato ya kodi binafsi, bila upungufu wowote, wakati mjadala unaendelea bungeni.


Serikali inahitaji kuwashawishi maseneta wa vyama vingine, kupitisha muswada wake kwa ukamilifu, kwa sababu chama cha Labor kina ongoza kampeni ya kugawa muswada huo.

Wiki ijayo, seneti ita endelea na mjadala kuhusu mpango unao salia wa makato ya kodi kwa biashara ambayo serikali imependekeza. Makato hayo yatapunguza kiwango cha kodi ya makampuni kutoka 30% hadi 25%.

Mnamo mwezi Aprili, serikali ilikosa kura mbili tu, kupitisha muswada huo, na tangu wakati huo , seneta wa chama cha One Nation Pauline Hanson, amebadili msimamo wake waku isaidia serikali kupitisha muswada huo.

Wakati huo huo Seneta Brian Burston, aliye timuliwa kutoka chama cha One Nation, kuhusu swala hilo, amejiunga na chama kipya chakisiasa cha Clive Palmer na amesema ata tekeleza makubaliano aliyo fanya na seneta Cormann, kuunga mkono makato hayo ya kodi kwa ukamilifu.

Share
Follow SBS Swahili

Download our apps
SBS Audio
SBS On Demand

Listen to our podcasts
Independent news and stories connecting you to life in Australia and Swahili-speaking Australians.
Ease into the English language and Australian culture. We make learning English convenient, fun and practical.
Get the latest with our exclusive in-language podcasts on your favourite podcast apps.

Watch on SBS
SBS World News

SBS World News

Take a global view with Australia's most comprehensive world news service