Malcolm Turnbull amemshtumu waziri mkuu wa zamani Tony Abbott kwaku athiri kimakusudi utendakazi wa serikali ya mseto katika matokeo mapya ya kura ya maoni yaliyo chapishwa hivi karibuni.
Serikali ya mseto kwa sasa imeshindwa na chama cha Labor kwa alama 10, serikali ikiwa na 45% ya umaarufu wakati chama cha Labor kina 55% ya umaarufu miongoni mwa wapiga kura, kwa mujibu wa shirika la Newspoll ambalo lili chapisha matokeo yake katika gazeti la The Australian jumatatu tarehe 27 mwezi wa 2 2017.
Matokeo hayo niya chini zaidi kwa tokea Malcolm Turnbull alipo chukua wadhifa wa Bw Abbot katika serikali ya mseto.
Share
