Hatua ya serikali ya Kenya kutoa muda huo wa wiki mbili kwa shirika la UNHCR kufunga kambi hizo za wakimbizi, imetafsiriwa kama iliyochochewa na mgogoro baina yake na Somalia.
UNHCR yapewa siku 14 kufunga kambi za Dadaab na Kakuma nchini Kenya

Participants join the queue for water and food distribution in Kakuma Refugee Camp, Kenya. (SBS) Source: SBS
Serikali ya Kenya imetoa muda wa siku 14 kwa shirika la umoja wa mataifa kuhusu wakimbizi UNHCR, kuzifunga kambi za wakimbizi za Daadab na Kakuma kufuatia vitisho vya kiusalama vinavyosababishwa na baadhi ya wakimbizi.
Share